Thursday, September 16, 2010

Nyani achekapo Kundule

Kwa asilimia 99 ya Watu weusi duniani na hususan Waafrika hakuna anayeweza kumcheka mwenzie katika masuala ya ngono na uzinzi. Tumekubuhu, Ukiona kuna wanaocheka basi wamithiishe na nyani achekaye kundu la mwenzie !

Uafrika hausimami bila ya mambo kama hayo. Vinginevyo huyo Mwafrika bandia. Jamani tuambieni ukweli kwani Der Spiegel llishafanya utafiti wenye mizizi toka kwa Sigmund Freud na tunayoona katika mizunguko yetu ya kila siku hapa hapa nchini.


Njia muafaka ni kukubali kuwa sisi sote tuko kama tulivyo na ndivyo tulivyoumbwa na kazi ianze kuoanisha maumbile yetu na kile kinachotakiwa. Maana ngono haizui kuwa na taifa imara kiuchumi na madhubuti katika ustawi wa jamii. Inawezekana kuchanganya raha zetu na karaha zetu, utamu na uchungu wetu, ubaya na uzuri wetu kisha tukapata kilicho bora na chenye baraka zaidi.