VIGOGO na Vizito nchini wanajua kinachotokea wanapoingia kwenye ndege kwenda majuu au kurudi nyumbani. Maisha ya kwenye ndege hufanana na yale ya huko nje kunakoitwa kuliko endelea.
Kwa bahati nzuri au mbaya wakubwa wanaporudi Tanzania hupokewa na magari yao yenye viyoyozi na kupelekwa kwenye majumba yao ya kifahari au ofisi zao zenye viyoyozi wakaendelea na starehe nyumbani kama waliyokuwa nayo kwenye ndege na huko ugenini.
Mswahili wa Kariakoo, hata hivvyo, anayelazimika kupanda daladala uwanja wa ndege kurudi nyumbani huona ghafla karudia kwenye jalala lile lile alilotoka.
Jambo hili, lipo, linaendelea na hakuna kiongozi ambaye kwa mamia ya safari zake nchi za nje ameshawahi kuinufaisha nchi na wananchi wakawa na hali nafuu zaidi ya ile waliyokuwa nayo kabla ya safari zake.
Huondoka, wakenda, wakarudi na kichwani hakuna kitu (sifuri kabisa) kuhusiana na kuinua miji na nchi yao ikafanana fanana anagalau na kule wanakotoka. Bila shuka wanapofika huko hufunga macho na masikio yao na wakaishiwa kudanganywa kwa hili na lile, kama sio kukubali kuwa Mwafrika kamwe hawezi kuwa na maisha kama ya mzungu chini ya uongozi kama wao.
Monday, January 9, 2012
Hoteli za Kiswahili na utu wa mzawa...
SERA za kitalii zinazohakikisha kwamba hoteli ya kitalii ina vyoo na maliwato zenye tailzi, zinazonukia vizuri na safi wakati wote lakini zinashindwa kuchangia mabadiliko ya hoteli za Kiswahili ingawa zikawa na huduma ya vyoo safi sio sera zinazojali uhai na ubora wa maisha ya mzawa na mwananchi.
Ni sera za seramala kukalia maboksi au magogo au la mfinyanzi kuacha mkewe akipikia vigae. Na viongozi wasio na habari kwa kinachotokea kwa mamilioni ya watu wao, lakini wakawa wanataka kujua kila kitu kinachowatokea wazungu kumi au mia waliopo nchini sio viongozi wanaoweza kuipeleka nchi popote pale pa kujivunia.
Ni sera za seramala kukalia maboksi au magogo au la mfinyanzi kuacha mkewe akipikia vigae. Na viongozi wasio na habari kwa kinachotokea kwa mamilioni ya watu wao, lakini wakawa wanataka kujua kila kitu kinachowatokea wazungu kumi au mia waliopo nchini sio viongozi wanaoweza kuipeleka nchi popote pale pa kujivunia.
Rasilimali asili na wazawa ni bora kuliko wawekezaji na mitaji toka nje.....
NADHARIA zinazozaliwa nyumbani badala ya kutoka ugenini, aghalabu, kwa wakoloni zinatoa umuhimu wa juu kabisa katika kuwathamini wazawa kama rasilimali endelevu na ya kudumu kwa maendeleo ya nchi inayokusudia kuwa huru kikwelikweli.
Nadharia hii inatoa kipaumbele kwa rasilimali nyumbani zaidi kuliko rasilimali azimishi. Mantiki ikiwa cha nje huweza kuondolewa wakati wowote, lakini cha ndani hakiwezi kuondolewa chote.
Sera zinazofuatwa na serikali kama ile ya Tanzania ni za kizamani na zenye mashiko yake toka kwenye ukoloni na haziwezi kamwe kuwa chachu ya maendeleo ya nchi hiyo.
Sera hizi ni zile zinazolazimisha kumpa mtu mshahara mkubwa tu eti kwa sababu ni mwanasiasa au mtumishi wa serikali bila kuoanisha mchango wa mhusika na maendeleo yanayoonekana na kukubalika katika eneo husika.
Halafu kama vile kwa kuambizana serikali nyingi za Kiafrika kwa umasikini wao wa mawazo zimeridhia daktari alipwe mshahara mdogo kuliko mbunge asiyesoma kabisa; mwalimu alipwe ujira mdogo kuliko mkuu wa mkoa au wilaya anayevuruga na kurudisha nyuma eneo analotakiwa kuendeleza; au nesi kulipwa mshahara mdogo kuliko kiongozi wa kuteuliwa ambaye huishia kufanya mengi kwa manufaa yake binafsi na jamaa zake na siyo ya wananchi.
Nadharia ya kileo katika masuala ya kuthamini na kuheshimu zaidi rasilimali yetu wenyewe ina mapendekezo mbalimbali ya kuondokana na udhalimu huu wa miaka kadhaa. Mojawapo kubwa likiwa ni kwa wabunge katika mabunge na mabaraza yetu kulipwa mshahara kulingana na elimu na ujuzi walio nao na sio vinginevyo.
Aidha, watumishi wanaochangia waziwazi kuokoa maisha ya watu; kubadilili maisha na mwelekeo wa watu na nchi; na wote wanaoutmia nguvu au musuli zao, akili au maarfia yao, uwezo au vipaji vyao watakuwa wakipata mishahara mikubwa pengine kuliko wabunge na mawaziri. Na hivyo kuondoa uroho wa watu kukimbilia kuwa wabunge au mawaziri wakati uwezo hawana kwa sababu ya tamaa ya cheo na fedha tu.
Nadharia hii inatoa kipaumbele kwa rasilimali nyumbani zaidi kuliko rasilimali azimishi. Mantiki ikiwa cha nje huweza kuondolewa wakati wowote, lakini cha ndani hakiwezi kuondolewa chote.
Sera zinazofuatwa na serikali kama ile ya Tanzania ni za kizamani na zenye mashiko yake toka kwenye ukoloni na haziwezi kamwe kuwa chachu ya maendeleo ya nchi hiyo.
Sera hizi ni zile zinazolazimisha kumpa mtu mshahara mkubwa tu eti kwa sababu ni mwanasiasa au mtumishi wa serikali bila kuoanisha mchango wa mhusika na maendeleo yanayoonekana na kukubalika katika eneo husika.
Halafu kama vile kwa kuambizana serikali nyingi za Kiafrika kwa umasikini wao wa mawazo zimeridhia daktari alipwe mshahara mdogo kuliko mbunge asiyesoma kabisa; mwalimu alipwe ujira mdogo kuliko mkuu wa mkoa au wilaya anayevuruga na kurudisha nyuma eneo analotakiwa kuendeleza; au nesi kulipwa mshahara mdogo kuliko kiongozi wa kuteuliwa ambaye huishia kufanya mengi kwa manufaa yake binafsi na jamaa zake na siyo ya wananchi.
Nadharia ya kileo katika masuala ya kuthamini na kuheshimu zaidi rasilimali yetu wenyewe ina mapendekezo mbalimbali ya kuondokana na udhalimu huu wa miaka kadhaa. Mojawapo kubwa likiwa ni kwa wabunge katika mabunge na mabaraza yetu kulipwa mshahara kulingana na elimu na ujuzi walio nao na sio vinginevyo.
Aidha, watumishi wanaochangia waziwazi kuokoa maisha ya watu; kubadilili maisha na mwelekeo wa watu na nchi; na wote wanaoutmia nguvu au musuli zao, akili au maarfia yao, uwezo au vipaji vyao watakuwa wakipata mishahara mikubwa pengine kuliko wabunge na mawaziri. Na hivyo kuondoa uroho wa watu kukimbilia kuwa wabunge au mawaziri wakati uwezo hawana kwa sababu ya tamaa ya cheo na fedha tu.
Subscribe to:
Posts (Atom)
