NADHARIA zinazozaliwa nyumbani badala ya kutoka ugenini, aghalabu, kwa wakoloni zinatoa umuhimu wa juu kabisa katika kuwathamini wazawa kama rasilimali endelevu na ya kudumu kwa maendeleo ya nchi inayokusudia kuwa huru kikwelikweli.
Nadharia hii inatoa kipaumbele kwa rasilimali nyumbani zaidi kuliko rasilimali azimishi. Mantiki ikiwa cha nje huweza kuondolewa wakati wowote, lakini cha ndani hakiwezi kuondolewa chote.
Sera zinazofuatwa na serikali kama ile ya Tanzania ni za kizamani na zenye mashiko yake toka kwenye ukoloni na haziwezi kamwe kuwa chachu ya maendeleo ya nchi hiyo.
Sera hizi ni zile zinazolazimisha kumpa mtu mshahara mkubwa tu eti kwa sababu ni mwanasiasa au mtumishi wa serikali bila kuoanisha mchango wa mhusika na maendeleo yanayoonekana na kukubalika katika eneo husika.
Halafu kama vile kwa kuambizana serikali nyingi za Kiafrika kwa umasikini wao wa mawazo zimeridhia daktari alipwe mshahara mdogo kuliko mbunge asiyesoma kabisa; mwalimu alipwe ujira mdogo kuliko mkuu wa mkoa au wilaya anayevuruga na kurudisha nyuma eneo analotakiwa kuendeleza; au nesi kulipwa mshahara mdogo kuliko kiongozi wa kuteuliwa ambaye huishia kufanya mengi kwa manufaa yake binafsi na jamaa zake na siyo ya wananchi.
Nadharia ya kileo katika masuala ya kuthamini na kuheshimu zaidi rasilimali yetu wenyewe ina mapendekezo mbalimbali ya kuondokana na udhalimu huu wa miaka kadhaa. Mojawapo kubwa likiwa ni kwa wabunge katika mabunge na mabaraza yetu kulipwa mshahara kulingana na elimu na ujuzi walio nao na sio vinginevyo.
Aidha, watumishi wanaochangia waziwazi kuokoa maisha ya watu; kubadilili maisha na mwelekeo wa watu na nchi; na wote wanaoutmia nguvu au musuli zao, akili au maarfia yao, uwezo au vipaji vyao watakuwa wakipata mishahara mikubwa pengine kuliko wabunge na mawaziri. Na hivyo kuondoa uroho wa watu kukimbilia kuwa wabunge au mawaziri wakati uwezo hawana kwa sababu ya tamaa ya cheo na fedha tu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment