SERA za kitalii zinazohakikisha kwamba hoteli ya kitalii ina vyoo na maliwato zenye tailzi, zinazonukia vizuri na safi wakati wote lakini zinashindwa kuchangia mabadiliko ya hoteli za Kiswahili ingawa zikawa na huduma ya vyoo safi sio sera zinazojali uhai na ubora wa maisha ya mzawa na mwananchi.
Ni sera za seramala kukalia maboksi au magogo au la mfinyanzi kuacha mkewe akipikia vigae. Na viongozi wasio na habari kwa kinachotokea kwa mamilioni ya watu wao, lakini wakawa wanataka kujua kila kitu kinachowatokea wazungu kumi au mia waliopo nchini sio viongozi wanaoweza kuipeleka nchi popote pale pa kujivunia.
Monday, January 9, 2012
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment